Friday, December 6, 2013

mkutano wa makocha waandamizi kujadili mustakabali wa Taifa Stars waanza leo visiwani Zanzibar

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe ambaye bia yake inadhamini Taifa Stars, akitoa mada wakati wa ufunguzi wa mkutano unaojumuisha wataalamu mbalimbali kutoka Tanzania bara na Zanzibar ili kuangalia namna ya kuboresha Timu ya Taifa (Taifa Stars). Waliokaa kutoka kushoto ni Rais wa ZFA Ravia Idarous Faina, Rais wa TFF Jamal Malinzi, Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Zanzibar, Hamisi Said na Makamu wa Rais wa ZFA Ali Mohamed Ali. Mkutano huo wa siku tatu unaodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager unafanyika katika hoteli ya Mtoni Marine visiwani Zanzibar.
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Zanzibar, Hamisi Said (aliyekaa katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na jopo la makocha na wakufunzi maarufu nchini wanaokutana Visiwani Zanzibar kuangalia namna ya kuboresha Timu ya Taifa Taifa Stars. Wengine waliokaa kutoka kushoto ni Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager George Kavishe, Makamu wa Rais wa ZFA Ali Mohamed Ali, Rais wa TFF Jamal Malinzi, Rais wa ZFA Ravia Idarous Faina, mwenyekiti wa jopo hilo la wataalamu, Kanali mstaafu Idd Kipingu na Katibu wake Rutayuoga Pelegrinius.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
The Official Blog of Tanzania Football Federation