Friday, January 17, 2014

RAIS WA TFF AKITEUA KITUO CHA ALLIANCE ACADEMY KUWA KITOVU CHA MAANDALIZI YA U17 WA MWAKA 2019

ZIARA ya Rais wa TFF Jamal malinzi hatimaye imemelizika leo hapa jijini Mwanza kwa matukio mawili makubwa kufanyika.

Tukio la Kwanza limefanyika majira ya saa 2:30 katika ofisi za Halmashauri ya jiji la Mwanza ambapo Shirikisho hilo limesaini mkataba kati yake na Halmashauri hiyo kwaajili ya kuboresha uwanja wa Nyamagana.

Ili ipate kumwaga fedha zake za msaada kiasi cha dola laki 5 ambapo nyingine dola laki 1 zitatoka Halmashauri ya jiji la Mwanza, FIFA  ilikuwa ikitaka uthibitisho toka TFF kuwa uwanja huo kwa miaka yote utatumika kwa matumizi ya michezo yaani soka na si vinginevyo  kwaajili ya kuanza uboreshaji wa uwanja huo uliokuwa na utata wa kutaka kubadilishwa matumizi.

Tukio la pili Malinzi na timu yake ya wataalamu toka TFF, majira ya saa 4 asubuhi imetembelea na kukikagua kituo cha elimu na soka cha Alliance Academy ikiwa ni mwanzo wa mpango wa kitaifa wa kuwekeza katika soka la vijana.
Jamal Malinzi alipata fursa ya kuzungumza na wachezaji na wanafunzi vijana wanaochukua masomo ya usimamizi na uamuzi wa michezo (marefa), kikubwa sanjari na kuzingatia michezo pia alisisitiza kuiweka elimu mbele. 
Tofauti na eneo la kukaa watazamaji kwa kila kiwanja, katika eneo hili vimeunganika viwanja viwili vyenye ukubwa wa mita 100 kila kimoja (nazungumzia maeneo ya kuchezea) na kingine kilichopo eneo la mabweni ya wasichana, ambapo TFF kupitia rais wake Jamal Malinzi imeahidi kuvikarabati viwanja hivi kwa kuvisawazisha kwa greda, kuviwekea magoli ya kisasa, kuweka udongo wenye rutuba na kuviwekea nyasi za kupanda zenye kiwango.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
The Official Blog of Tanzania Football Federation