Sunday, November 3, 2013

JAMAL MALINZI AMTEUA BONIFACE WAMBURA KUWA KAIMU KATIBU MKUU TFF

Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemteua Bw. Boniface Wambura (kulia) kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa TFF. Uteuzi huo ni kuanzia Novemba 2 mwaka huu.

Aidha aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah (kushoto) ameagizwa aende likizo ya malipo hadi atakapomaliza mkataba wake.
 Kamati ya Utendaji inaviomba vilabu, vyama vya wilaya, vyama vya mikoa, vyama shiriki na wadau wote kumpa ushirikiano Bw. Boniface Wambura katika utekelezaji wa majukumu yake.
  
Jamal Malinzi
Rais TFF 


Dar es Salaam 
Novemba 3, 2013

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
The Official Blog of Tanzania Football Federation