Hatua ya robo fainali ya Kili Taifa Cup inaanza Mei 22 mwaka huu Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Robo fainali zitachezwa mechi
mbili kwa siku. Ya kwanza saa 8.00 mchana na ya pili saa 10.00 jioni.
Mei 22 mechi ya kwanza ni Singida (Kindai Shooting Stars) na Ilala. Mechi ya
pili ni Mwanza (Mwanza Heroes) na Arusha (Mount Meru Warriors). Mei 23 mechi ya
kwanza ni Mbeya na Ruvuma (Ruvuma Warriors) wakati ya pili ni timu ya Taifa
chini ya umri wa miaka 23 (U23) na Kagera (Lweru Eagles).
Nusu fainali ya kwanza itakayohusisha washindi wa robo fainali za Mei 22
itachezwa Mei 24. Ya pili itachezwa Mei 25 wakati Mei 26 itakuwa mapumziko.
Mechi ya mshindi wa tatu itakuwa Mei 27 na fainali itachezwa Mei 28.
Waamuzi watakaochezesha hatua hiyo ambao wote wana beji za Shirikisho la
Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ni Israel Mujuni, Judith Gamba na Oden Mbaga.
Waamuzi wasaidizi ni Samwel Mpenzu, Hamis Chan’gwalu, Saada Tibabimale, Zahra
Hussein, John Kanyenye na Erasmus Jesse.
Makamishna wa mechi ni Hakim Byemba na Mrisho Bukuku wakati mtathmini wa marefa
(referee assessor) ni Charles Mchau. Msimamizi wa fainali hizo ni Khalifa Mgonja
ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF).
0 comments:
Post a Comment