Wednesday, April 13, 2011

TBL pamoja TFF Wakutana na Wahariri wa Habari za Michezo kuzungumzia Kili Taifa Cup 2011

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro ambao ndio wadhamini wakuu wa Ligi ya Kili Taifa Cup 2011,George Kavishe akizungumza katika mkutano na Wahariri wa Habari za Michezo kutoka vyombo mbali mbali vya Habari juu ya mchakato mzima wa ligi ya Kili Taifa Cup 2011 utakavyokuwa,mkutano huu umefanyika mchana huu katika hoteli ya Paradise,Benjamin Mkapa jijini Dar.
Katibu Mkuu wa TFF,Angetile Osseah akijibu moja ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na Wahariri wa Habari za Michezo katika mkutano uliofanyika mchana huu katika hoteli ya Paradise,Benjamin Mkapa tower,jijini Dar.
Meneja Habari na Mahusiano wa kampuni ya Excutive Solutions,Mike Mukunza akitoa muongozo kwa Wahariri wa Habari za Michezo wa vyombo mbali mbali vya Habari juu ya namna habari hizo zitakavyotakiwa kuwa katika vyombo hivyo.
Afisa wa Idara ya Ufundi (TFF),Saad Kawemba akijibu moja ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na Wahariri wa Habari za Michezo.
Mkurugenzi wa Masoko wa TFF,Jimmy Kabwe,akizungumza katika mkutano huo.
Meza Kuu ikisikiliza maswali toka kwa wahariri wa Habari za Michezo.
Maulid Kitenge wa ITV/Radio One akiuliza swali kwa viongozi wa TFF.
Zubeiry Ismail wa Tanzania Daima akiuliza swali.
Mpangilio wa Mikoa katika Ligi ya Taifa.
Mkutano ukiendelea.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
The Official Blog of Tanzania Football Federation