Friday, April 8, 2011

MAPATO MECHI YA AFRICAN LYON vs YANGA


Mechi namba 125 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya African Lyon na Yanga iliyochezwa Aprili 7 mwaka huu Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam imeingiza sh. 22,252,000.

Mapato hayo ni kutokana na watazamaji 4,476 waliolipa kutazama mechi hiyo.
Viingilio katika pambano hilo vilikuwa sh. 15,000 kwa VIP, sh. 8,000 Jukwaa
Kubwa, sh. 5,000 Jukwaa la Kijani n ash. 3,000 Mzunguko.

Baada ya kuondoa asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 3,394,372.88 fedha iliyobaki kwa mgawanyo kwa pande zote husika ni sh. 18,857,627.12.

Jumla ya gharama za awali za mchezo ni sh. 5,185,200 wakati kila timu ilipata
sh. 4,101,728.14. Uwanja sh. 1,367,242.71, TFF sh. 1,367,242.71, gharama za mchezo sh. 1,367,242.71, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 136,724.27, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 546,897.08 na Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 683,621.36.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
The Official Blog of Tanzania Football Federation