Tuesday, March 22, 2011

U23 KUONDOKA MACHI 24

Msafara wa timu ya U23 wenye wachezaji 18 kwenda Cameroon utaondoka Machi 24 mwaka huu kwa ndege ya Kenya Airways ukiongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Athuman Kambi.

Wachezaji hao ambao wako chini ya Kocha Jamhuri Kihwelo na msaidizi wake Ayoub Mohamed ni Jamal Mnyate, Salum Telela, Omega Seme, Mussa Gharib, Cosmas Lewis, Abdulrahim Shaaban, Zahoro Pazi, Issa Rashid, Himid Mao, Salum Abubakar, Mcha Khamis, Amour Suleiman, Samuel Ngasa, Shomari Kapombe, Babu Ally, Bakari Hamis, Faraji Kabali na Thomas Ulimwengu.

Wengine kwenye msafara huo ni Meneja wa Timu, Mohamed Rishard, Daktari wa Timu, Dk. Joachim Mshanga na mtunza vifaa (Kit Manager), Edward Venance.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
The Official Blog of Tanzania Football Federation