akimtoka beki wa timu ya Afrika ya kati, Manga David.
Stars baada ya kuifunga Afrika ya Kati.
Taifa Stars imeifunga kishujaa timu ya taifa ya Afrika ya Kati bao 2-1 katika mechi ya awali kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika mwakani uliofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam na kushuhudiwa na maelfu ya wapenzi wa soka.
Mechi hiyo ya vuta nikuvute ambayo Stars iliahitaji ushindi ili kujiweka sawa katika mbio hizo za kuwania fainali hizo zitakazofanyika Gabon na Equatorial Guinea, ilishuhudia wenyeji wakipigwa bao mo9ja katika kipindi cha kwanza.
Stars ilisawazisha dakika ya 49 Shaaban Nditi wakati bao la ushindi liliwekwa kimiani na Mbwana Samatta dakika ya 89.
Stars ilicheza mechi ya kwanza na Algeria na kutoka sare ya bao 1-1 kabla ya kufungwa bao 1-0 na Morocco nyumbani.
Ushindi wa mechi ya leo umerejesha imani ya Tanzania kusonga mbele.
Taswira zinakuja baadaye kidoooogo....
0 comments:
Post a Comment