Kamati ya Mashindano chini ya Mwenyekiti wake Makamu wa Pili wa Rais wa TFF, Ramadhan Nassib ilikutana Machi 19 mwaka huu na kupitia taarifa za mashindano mbalimbali. Miongoni mwa matukio yaliyoripotiwa na waamuzi na makamishna yaliyofikishwa kwenye kamati hiyo yalihusu mechi za Ligi Kuu ya Vodacom.
Mechi namba 86 kati ya Majimaji na Yanga iliyochezwa Februari 5 mjini Songea, ripoti ilionesha kuwa wachezaji wa Yanga walivunja viti katika Uwanja wa Majimaji, kuvunja mlango wa Mama Lishe na washabiki wake kutaka kuvamia waamuzi baada ya mchezo.
Kocha wa Toto African, Choke Abeid alimtukana mwamuzi wa mezani matusi ya nguoni na kutupa chupa ya maji chini katika mechi namba 95 dhidi ya Simba iliyochezwa CCM Kirumba, Mwanza. Kwa kitendo hicho mwamuzi alimuondoa kwenye benchi la wachezaji.
Katika mechi namba 96 iliyochezwa Bukoba kati ya Kagera Sugar na Yanga, wachezaji wa Kagera, Msafiri Devo na David Luhende waliwarushia waamuzi chupa za maji na kutoa matusi ya nguoni.
Naye kipa wa Mtibwa Sugar, Shabani Kado ameripotiwa kumtukana matusi ya nguoni mwamuzi kwenye mechi namba 103 dhidi ya Toto Africans iliyochezwa Mwanza ambapo alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Licha ya kanuni kueleza adhabu kwa makosa hayo, kujirudia mara kwa mara na mengine kufanyika nje ya uwanja, Kamati ya Mashindano imeyaandikia taarifa na kuyawasilisha kwenye Kamati ya Nidhamu ikipendekeza adhabu zaidi kwa wahusika.
Mechi namba 86 kati ya Majimaji na Yanga iliyochezwa Februari 5 mjini Songea, ripoti ilionesha kuwa wachezaji wa Yanga walivunja viti katika Uwanja wa Majimaji, kuvunja mlango wa Mama Lishe na washabiki wake kutaka kuvamia waamuzi baada ya mchezo.
Kocha wa Toto African, Choke Abeid alimtukana mwamuzi wa mezani matusi ya nguoni na kutupa chupa ya maji chini katika mechi namba 95 dhidi ya Simba iliyochezwa CCM Kirumba, Mwanza. Kwa kitendo hicho mwamuzi alimuondoa kwenye benchi la wachezaji.
Katika mechi namba 96 iliyochezwa Bukoba kati ya Kagera Sugar na Yanga, wachezaji wa Kagera, Msafiri Devo na David Luhende waliwarushia waamuzi chupa za maji na kutoa matusi ya nguoni.
Naye kipa wa Mtibwa Sugar, Shabani Kado ameripotiwa kumtukana matusi ya nguoni mwamuzi kwenye mechi namba 103 dhidi ya Toto Africans iliyochezwa Mwanza ambapo alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Licha ya kanuni kueleza adhabu kwa makosa hayo, kujirudia mara kwa mara na mengine kufanyika nje ya uwanja, Kamati ya Mashindano imeyaandikia taarifa na kuyawasilisha kwenye Kamati ya Nidhamu ikipendekeza adhabu zaidi kwa wahusika.
0 comments:
Post a Comment